Pages

Saturday, November 24, 2012

"Midomo yangu itapiga vigelegele kwa shangwe" - Zaburi 71:23

Kazi ya Yeremia ya kujenga na kupanda ilizaa matunda. Wayahudi fulani na vilevile watu wasio Waisraeli waliokoka kuharibiwa kwa Yerusalemu mwaka 607 Kabla ya Wakati wa kawaida.     Tunajua kuhusu Warekabu, Ebedmeleki, na Baruku. (Yeremia 35:19 ; Yeremia 39:15-18 ; Yeremia 43:5-7) Marafiki hao wa Yeremia waliokuwa washikamanifu na wenye kumwogopa Mungu, wanafananisha vizuri leo wale walio na tumaini la kuishi duniani, ambao wanasitawisha urafiki na jamii ya Yeremia. Jamii ya Yeremia inafurahia sana kuujenga kiroho 'umati mkubwa'. (Ufunuo 7:9) Vivyo hivyo, waandamani hao washikamanifu wa watiwa-mafuta wanafurahi sana kuwasaidia watu wenye mioyo minyoofu kupata ujuzi juu ya kweli. Watu wa Mungu wanaelewa kwamba kuhubiri habari njema si huduma tu ya hadharani kwa wale wanaosikia ujumbe huo, bali pia ni tendo la ibada kwa Mungu wetu. Iwe watu watatusikiliza au hawatatusikiliza, kumtolea Yehova utumishi mtakatifu kupitia kazi yetu ya kuhubiri, kunatuletea shangwe kubwa - Warumi 1:9.